Categories
Uncategorized

Mkutano na wanajamii kwa ajili ya kutengeneza mpango wa kupambana na mafuriko

Mkutano ulifanyika kwenye mitaa miwili ya kata kigogo kama majaribio ili kuona ni jinsi gani taarifa za wanajamii zinaweza kuutumika kutengeneza mpango huu.

Picha; Mkutano na Wana jamii.

Tarehe 26 mwezi wa tatu 2018, Timu ya HOT Tanzania ilifanya mikutano ya majaribio kwenye mitaa ya Mbuyuni na Kigogo kati. Lengo kubwa la mkutano ilikuwa kuhamasisha majadiliano na wadau mbalimbali kama Mtendaji wa mtaa, Mwenyekiti wa mtaa Wajume, Asasi zisizo za kiserikali na mashirika ya kijamii kama Tegemeo. (Tegemeo ni shirika linalotoa elimu kwa jamii kwenye mambo ya elimu ya mazingira na kusaidia yatima- Inafanya kazi nchi nzima.

Kwenye mkutano huu, Wanajamii walionyesha maeneolvitu ambavyo wanaona vina thamani sana kwenye mitaa yao. Taarifa hizi zitawezesha Ramani Huria kutengeneza mpango wa kupambana na mafuriko. Ramani hizi zitakuwa ni zao lililotokana na taarifa zilizokusanywa wakati wa mkutano na kupangiliwa kwa kutumia programu ya huru kama QGIS.

Picha- Viongozi wa mtaa wanasoma ramani na kuonyesha makazi yao.

Ninafurahi kuwa sehemu ya zoezi, Kujua nini kinaendelea kwenye mtaa wangu, kushiriki kwenye kutambua maeneo salama na yasiyo salama kwa kutumia ramani ni mwanzo mruri ili kutengeneeza mpango wa kupambana na mafuriko” Mazoea Ling’omba- Mjumbe, Mtaa wa Kigogo Kati.

Mkutano ulihudhuriwa na washiriki 43 kutoka mitaa miwili, kwa mikutano shirikishi iliyo huisha makundi ya watu wanne hadi watano. Zoezi lilianza kwa kuwaelekeza washiriki jinsi ya kusoma ramani, kuonyesha maeneo muhimu na kuonyesha makazi yao. Mwisho wa majadiliano washiriki waliweza kuonyesha nyumba zao na kuongeza majina ya mitaa ambapo kulikuwa hakuna taarifa au hazikuwa sahihi.

Picha; Ramani zinaboreshwa kwa kuongeza taarifa zilizo kosekana, maeneo hatarishi yana onyeshwa kwa vitu muhimu kwenya mtaa..

Najivunia kuwa sehemu ya mchakato huu- Nimepewa  mafunzo ya jinsi ya kusoma ramani, na kuweka vitu muhimu kwenye ramani kuboresha taarifa kwa ajili ya kupambana na mafuuriko” Miraji Simba- Mratibu Red Cross.

Somo muhimu lililo jifunzwa kutoka kwenye warsha hii ni kuwa wanajamii ndio watu muhimu katika kutengeneza mpango huu. Wao wanaweza kutoa historia na mwenendo wa mafuriko na kuonyesha maeneo yaliyo kwenye hatari ya kupata mafuriko ( Kwa mfano mhandisi angeweza kujua ni wapi kuna mafuriko kwa kutumia mahesabu, lakini hawezi kutoa wigo historia na athari halisi za mafuriko)- Taarifa walizotoa wanajamii zinaonyesha mwonekano halisi na mwenendo wa mafuriko na kutoa uelewa zaidi wa jinsi mafuriko yalivo badilika kulingana muda.

Wana jamii na viongozi wa kata walijihakikishia na walikuwa na furaha kuhusu mradi huu pale waliposikia kuwa mpango huu wa kupambana na mafuriko hauhusishi kuwahamisha kwenye makazi yao bali kutengeneza mpango mzuri wa jinsi ya kupunguza mafuriko na na mateso yatokanayo na athari za mafuuriko.

Mwanzoni mimi na jirani zangu tulipta wasiwasi kuwa nyumba zetu zitabomolewa, lakini sasa tuna amani kwa  kuwa mradi umeelezwa vizuri kwetu. Nitaenda kuwaelezea “watu wangu” kwenye shina ili kuwahakikishia kuwa mradi huu ni kwa ajili ya mpango wa kupambana na mafuriko na si kuvunja nyumba”Mjumbe-(jina limehifadhiwa).

Kwenye mitaa hii miwili, matatizo yote yaliyo onyeshwa na wana jamii yanafanana kwa sababu Kata nzima ya kigogo ipo kati ya mito miwili mikubwa- mto  Msimbazi na Kibangu ambayo ni mito “maarufu” inayosababisha mafuriko. Ni wazi kuwa mpango huu wa kuzuia mafuriko unalenga kwenye kuweka mapendekezo ya wana jamii ya vitu vya muhimu ambavyo vipo kwenye hatari ya kupata mafuriko na historia ya maeneo yanayopata mafuriko- Mpango ulioboreshwa wa kupunguza athari za mafuriko unaweza kutengenezwa.

Categories
Uncategorized

Ramani Huria

Tangu  2015, Ramani Huria imekuwa ikipambana na mambo yanayohusu mafuriko jijini Dar es salaam ili kupunguza mafuriko na kuhamasisha usimamizi endelevu wa rasilimali maji.Sasa tupo kwenye awamu ya pili  ya mradi, Ramani Huria 2.0 imejikita kwenye kutengeneza ramani ya kata za Dar es salaam zilizo kwenye hatari zaidi ya mafuriko, kama vile Kigogo na Hananasif, ili kutengeneza taarifa za mafuriko ambazo baadaye zitatumika kufanya maamuzi na mipango ya kupunguza mafuriko. Timu ya Ramani Huria huanza kwa kujitambuisha kwa maofisa wa kata, kwa kuelezea mradi na kupewa baruua ya utangulizi kupeleka kwa watendaji wa mitaa. Baada ya hapo team itatambulishwa kwa wajumbe- viongozi wa ngazi ya chini kabisa kwenye serikali ya mtaa.  

Wiki hii tulitetembelea timu inayokusanya taarifa kuona kazi nzuri inayofanywa na timu hiyo. Tulifurahi kukutana na mwanajamii aliyeshiriki kwenye mradi wa Ramani Huria 1.0.

 ‘’Nilishiriki kwenye Ramani Huria 1.0 wakati tulikuwa tunatumia karatasi na GPS kuzunguka kukusanya taarifa. Ilikuwa inachukua muda mrefu na taarifa nyingine zinaweza kupotea kwenye mchakato, Lakini sasa kwa kuwa tunatumia simu kukusanya taarifa, inakuwa haraka na sio rahisi kwa taarifa kupotea’’ Hafidhi Hamza, wanajamii.

   

KUSHOTO; Mahojiano na mwanajamii aliyeshiriki kwenye mradi wa Ramani Huria 1.0.

KULIA; Mtaro ulioziba kutokana na uchafu nyuma ya nyumba ya mkazi kata ya Kigogo.

Taaarifa zinazokusanywa na ramani huria zinawasaidia wafanya maamuzi kwenye ngazi zote za kijamii kwenye hatua za kupunguza mafuriko kwenye maeneo yenye hatari ya mafuriko.Kulingana na ramani ambazo zilichapishwa kwenye ramani huria 1.0 tayari wanajamii wanaanzisha njia za usimamizi wa taka kusafisha mitaro iliyoziba na kuelimisha wakazi juu ya adhari za kutupa taka hovyo. Idadi ya watu inaongezeka na taka zinazozalishwa zinaongezeka maradufu, Ramani kama zinazotengenezwa na timu ya Ramani Huria ni muhimu kukuza ufahamu wa mafuriko, sababu za kupunguza na mipango ya majibu endapo mafuriko yatatokea.

Timu ya Ramani Huria ilianza kwa kutumia programu ya OpenMapKit kukusanya taarifa za kata ya Hananasif na sehemu ndogo ya kata ya kigogo. Timu hiyo iligundua kuwa ni ngumu zaidi kuchambua data zilizokusanywa katika muundo wa poligoni, hasa wakati wa kutengeneza Heat maps kunahitaji taarifa ya kukusanywa kama pointi, hivyo timu hiyo ikaanza kutumia Open Data Kit (ODK). ODK inaruhusu kukusanya pointi za taarifa na kujaza utafiti ili kuonyesha mwenendo wa mafuriko katika kata hii.

Mchakakato wa kukusanya taarifa ni kama ufuatao-

Mjumbe wa nyumba kumi atachagua mwanajamii mwenye simu ya kkidigitali ili:

  1. Simu itawekwa programu ya ODK.
  2. Kuhahakikisha kuwa dodoso limepakuliwa kutoka kwenye mtandao wa  www.turkus.net (Dodoso mara nyingi linakuwa kwenye lugha ya kiswahili ili kuepuka vikwazo vya lugha)
  3. GPS ya simu inatakiwa ikaguliwe (mara nyingi inatakiwa iwe na usahihi usiozidi mita 4)
  4. Mwanajammii ataelekezwa na timu ya Ramani Huria jinsi ya kukusanya taarifa kutumia ODK.
  5. Wanajamii wataelekezwa jinsi ya kufanya dodoso ili wawze kukusanya taarifa zinazohitajika.

Baada ya kuhakikisha kuwa wanajamii wamepata ujuzi unaohitajika kwenye kukusanya taarifa, kazi inaanza. Mwanajamii atapewa vocha ya simu ili ajiunge kwenye mtandao na power bank ili kuchaji simu endapo itahitajika.

 

PICHA; Mwanajamii na mjumbe wakikusanya taarifa kwenye programu ya ODK

“Ramani Huria 2.0 ni nzuri kuliko Ramani Huria ya mwanzo kwa sababu hii ya sasa tunakusanya taarifa kwa njia ya dodoso na mwanajamii anaulizwa kama nyumba yayke imewahi kupata mafuriko au laa. Hii inaweza kutoa taarifa za kuaminika na kumbukumbu kwa serikali” 

Hafidhi Hamza, Mwanajamii.

Timu pia ilionyesha jinsi inavyochambua taarifa zilizokusanywa ili kuhakikisha kuwa kila kitu kimekamilika kabla ya kuuhamia kwenye kata nyingine. Takwimu zinaonyeshwa kwa mujibu wa mjumbe kwenye eneo lake la kuongoza, na katika kila kifungu unaweza kujua kuwa dodoso limekamilika au laa.

Data za wajuumbe kata ya kigogo zikionyeshwa kwenye ramani- Kila kundi la rangi linaonyesha mipaka ya shina la mjumbe.

Timu pia inaweza kuangalia vizuri jinsi washiriki walivyojiibu maswali ya historia ya mafuriko kwenye maeneo yao. Washiriki wanaulizwa maswali kama “Je uliwahi kupatwa na mafuriko” “Mafuriko yalikuwa na kina gani”, “Je ulihama makazi yako kutokana na mafuriko” “unadhani nini kilisababisha mafuriko”

Timu ya kujenga taarifa mpya kwa kila mwaka mafuriko yanaripotiwa kwa sababu athari za mafuriko zinaweza kuonekana kwa urahisi zikichambuliwa kwa kila mwaka.

PICHA; Fomu ya uchunguzi wa ODK kuhoji kina cha mafuriko

Ramani kama hizo hapo juu zinaonyesha maeneo yaliyohatari kwa mafuriko. Tayari, faida za Ramani Huria 1.0 zinaweza kuonekana. Wajumbe wa shina walielezea jinsi ramani za RH 1.0 zimetumiwa kuwajulisha mipango ya kusafisha mitaro ili kuondoa taka kutoka kwenye mifereji. Kuongezewa kwa mipaka ya Wajumbe na taarifa sahihi zaidi ya kina za mafuriko kutoka kutoka Ramani Huria 2.0 itaendelea kuwajulisha na kuwashauri wanajamii na viongozi wa serikali juu ya maeneo ya kuzingatia katika mipango ya kupunguza mafuriko.

This week we visited the field team this week to see the amazing work that is being done by the team.We were excited to meet one of the community members who has been involved in mapping since 2015 when Ramani Huria 1.0 was implemented.

“I participated in Ramani Huria 1.0 when we were using field papers and GPS devices to move around to collect information. It was time consuming and you may have lost data during the process, but now that we’re using smartphones to collect data it’s quicker and you’re not likely to lose data in the process” – Hafidhi Hamza, Community Member

   

LEFT PHOTO; Interview with Community Mapper from Ramani Huria 1.0

RIGHT PHOTO; Drainage blockage caused by littering behind a resident’s house in Kigogo Ward

The data collected from Ramani Huria is helping inform decision makers at all levels of society on flood mitigation measures to tackle current pain points. Already, based on the printed maps produced from Ramani Huria 1.0, local people are establishing waste management initiatives to clean blocked drains and educate residents on the detrimental impact of littering. As population increases and the level of waste produced multiplies, maps such as those produced by the Ramani Huria team are imperative to raising awareness of flood causes, mitigation measures and response plans. The Ramani Huria team initially started to use OpenMapKit for data collection and mapped Hananasif ward and part of Kigogo ward. The team then realised that it is more difficult to analyse data collected in polygon format, especially when producing heat maps you need the data to be collected as points, so the team immediately switched to using Open Data Kit (ODK). ODK allows them to collect data points and fill out the survey to establish the trend of flooding in this particular ward.

The data collection process was conducted in the following manner –

Ten cell leaders (Wajumbe) would select a community member who owned a smartphone so that:

  1. The phone could be installed with Open Data Kit (ODK) Collect.
  2. They could make sure that the survey form is downloaded from the server; www.turkus.net (the survey is written in Swahili to avoid language barriers and is user friendly).
  3. The GPS accuracy of the device could be checked (usually less than 4 meters).
  4. A community member could be trained by the Ramani Huria team on how to collect data using ODK
  5. ODK questions will be elaborated to community members to make sure they collect the desired information.

After making sure that community members are equipped with the data collection skills needed, field work commences. A community member is provided with scratch cards (to buy internet packages) and a power bank.

 

PHOTOS; Community member and Mjumbe conduct ODK flood extent surveys with local residents

[symple_testimonial by=”” fade_in=”false”] “Ramani Huria 2.0 is far better than RH1 because in this phase we conduct community surveys and a community member is asked questions such as if the residents of a particular house had experienced flooding or not. This can provide reliable and documented information to the government” – Hafidhi Hamza, Community Member[/symple_testimonial]

The field team then demonstrated how they analyse field data to make sure that everything has been covered before moving on to the next ward. Data is visualized according to Mjumbe leaders area of jurisdiction and within each cluster you can determine if all of the survey questions have been covered.

SCREENSHOT; Kigogo Ward Mjumbe data points visualized on a map – each colour cluster represents a Mjumbe Shina boundary

The team are also able to visualize clearly respondents answers to questions about the history of flooding in their area. Respondents are asked questions such as, “have you ever experienced flooding?”, “how deep was the flood water?”, “have you moved settlement because of flooding?”, “what do you think caused the flooding?”.

The team create a new dataset for each year flooding is reported so that flood impact can easily be visualized by year.

PHOTO; ODK survey form questioning the depth of flooding

Maps like the one above demonstrate clearly areas prone for flooding. Already, the impact of Ramani Huria 1.0 can be seen. Community members explained how the RH 1.0 maps have been used to inform community cleanup initiatives to remove waste from blocked drains. The addition of Mjumbe boundaries and more accurate, detailed flood data from ODK from Ramani Huria 2.0 will continue to inform and advise community members and government officials on focus areas for flood mitigation planning.

Categories
Uncategorized

Wanafunzi na walimu wa chuo kikuu cha ardhi wafariwa mafunzo juu ya urasmishaji wa makazi

Ujanibishaji wa sasa unafanyika ili kurasmisha makazi yasiyo rasmi ya Dar es Salaam ambayo sasa inafikia asilimia 70 ya jiji. Kurasimisha makazi kunasaidia kutoa uhalali kwa jamii na kuongeza usalama wa umiliki wa wakazi na haki zao za ardhi. Kujenga makazi pia kunaruhusu mipango zaidi ya kudumu ya mji. Kwa bahati mbaya, mbinu za sasa za ukusanyaji wa taarifa kuelewa mipaka hii imesababisha taarifa zisizo sahihi kutokana na ushiriki mdogo wa wanajamii.

Ili kusaidia kuboresha mbinu za kukusanya taarifa za sasa zinazohitajika kwa ujanibishaji, timu ya HOT  Tanzania imetoa siku tatu za mafunzo na wanafunzi 6 wa elimu ya juu (Masters) wote wakijifunza Mipango na Usimamizi wa Mjini (Msc UPM), na wafanyakazi/wahadhiri 3 wa Chuo hicho. Hadi sasa, mbinu iliyochukuliwa kwenye ramani ya makazi yasiyo rasmi inahusisha matumizi ya picha za drone na satellite ili kutambua mipaka ya makazi. Utaratibu huu sui sahihi, hutumia muda mrefu kwa kuwa  watu wa ndani wamezoea picha za 3D (urefu, upana mna kimo) kila siku za nyumba zao kwenye barabara za mitaani, sio picha ya 2D ya drone (yenye urefu na upana) iliyochukuliwa kutoka juu. Maeneo yenye wakazi wengi pia hufanya kuwa ngumu kutambua nyumba za mtu binafsi na kufafanua mipaka.

Profesa Tumsifu Jonas Nkya (kulia), Daktari(Phd) John Lukenangula (kushoto) wakipakua na kujifunza kutumia Open Data Kit (ODK) kwenye mafunzo kutoka kwa mtaalamu kutoka Ramani Huria Iddy Chazua (Katikati).

Kwa tumaini la kuongeza ushiriki wa jamii na usahihi wa taarifa, timu ya HOT imewafundisha wanafunzi na wafanyakazi kuhusu ramani ya wazi ya jamii. Mafunzo yalihusisha jinsi ya kutumia OpenStreetMap (OSM), JOSM, OpenDataKit (ODK), na OpenMapKit (OMK), (programu za kutengeneza ramani zianzowekwa kwenye simu ili kukusanya taarifa). Kutumia zana hizi, tafiti za kidigitali zinaweza kukusanya taarifa katika ngazi ya mitaa kwa kuzungumza na wenyeji kutambua matumizi ya ardhi, umiliki na matumizi ya majengo, na hali ya kijamii na kiuchumi ya wenyeji. Kuweka sifa ya jengo kwenye OpenMapKit wakati wa kufanya tafiti ya ardhi kutakikisha kuwa matumizi ya ardhi yanaweza kufafanuliwa kwa usahihi zaidi. Kisha taarifa hii inaweza kutumika kupangilia mipaka ya makazi. Njia hii ni ya haraka zaidi na rafiki kwa mazingira zaidi kuliko tafiti za awali za karatasi na hatua ya ziada ya kuingiza taarifa inatolewa kutoka kwenye mchakato. Kwa kuhusisha wanajamii moja kwa moja katika mchakato wa ramani katika muundo ambao wanaweza kuhusishwa, taarifa sahihi zaidi hukusanywa. Wakati ramani ya jamii ikianza, Shina la mtaa (mgawanyiko wa viongozi wa mtaa), Wajumbe, wataongozana na timu ya kukusanya taarifa ili kuzungumza na wenyeji wa eneo kuwahakikishia lengo la mradi.

Mafunzo kwa vitendo kwa kuongozwa na Ivan Gayton, Meneja wa HOT Tanzania.

Ramani zilizotengenezwa kupitia mradi huu zitaweza kupatikana kwa kila mtu mtandaoni kupitia jukwaa la OpenStreetMap. Hii ina maana kwamba kwa mara ya kwanza, wenyeji wa makazi yasiyo rasmi watakuwa kwenye ramani na wanaweza kuingizwa zaidi na kushiriki katika mipango ya baadaye ya mji wao. Ramani zilizochapishwa zitatumika kama kuchora Mipango ya Mji ambayo itajifunza hali zilizopo za jiji na matumizi ya ardhi na kutafakari ambapo rasilimali zinapaswa kupewa au maeneo gani yanahitaji maendeleo. Ramani pia itasaidia kufuatilia mabadiliko katika matumizi ya majengo, kwa sasa, viongozi wa serikali hawana uhakika wa matumizi ya majengo ikiwa mtu anaomba idhini ya kubadilisha kazi ya jengo.

Baadhi ya wanafunzi walioshiriki kwenye mafunzo walikuwa na haya ya kusema:-

“Ramani za kijamii zinaweza kuongeza ushiriki wa jamii na na kutengeneza ramani za  mali zao na kuwashirikisha katika kukusanya taarifs yoyote ambayo ni muhimu kwa shughuli za kuimarisha/kurasmisha makazi” – Luteranya Mapambano mwanafunzi katika taaluma ya mipango miji. 2017/18.

“Ramani ya Jumuiya ni chombo muhimu katika kupunguza muda wa kazi wakati wa kuimarisha/ kurasimisha, kwa kuwa mtu yeyote anaweza kupata taarifa muhimu kama maendeleo na vipengele vingine bila umuhimu wa kwenda kwenye eneo husika” – Jikora, Emmanuel, Mwanafunzi katika taaluma ya mipango miji. 

Categories
Uncategorized

Hisia Za Kwanza/ Mwanzo Ramani Huria

Kwa sasa asilimia 70 ya miundombinu Dar es Salaam haijapangwa, maana yake ni kwamba miundo mara nyingi hujengwa katika maeneo ya mafuriko na haijatengenezwa kwa kutosha ili kukabiliana na maji mengi. Mara nyingi, hata majengo yasiyopangwa yaliyo ‘salama’ na mafuriko yana athari kubwa juu ya eneo jirani; Mpango usiofaa umesababisha ongezeko la udongo mgumu (Compact soil), ambao una viwango vya chini vya kunyonya maji ili kuzuia kusambaza maji wakati wa mafuriko.

Ramani Huria ni mradi unaofanywa na HOT, kwa lengo la kuzalisha ramani kwa nia kuu ya kuboresha mipango ya ustawi wa mafuriko na kuongeza ufahamu wa maeneo salama kwa watu wa eneo. Hii inamaanisha kuwa nyumba za baadaye zitajengwa katika maeneo salama na hatua hizo zinaweza kuchukuliwa ili kuimarisha au kuhamisha majengo ambayo sasa yana hatari. Aidha, inaweza kupunguza hatari ya kolera na kuzuia uhamisho wa ghafla.

Amelia Hunt – Mkufunzi wa Ramani na Msaidizi wa Mradi, HOT – na Zac Hill – Mshauri, Wote wamefika Dar es Salaam na wamekaa siku mbili za mwisho katika ofisi ya HOT iliyopo  dLab. Katika chapisho hili la blog wanaelezea yale waliyojifunza kuhusu mradi wa Ramani Huria kwa kuzungumza na wana timu.

Chapisho hili la blogu limeshuka katika sehemu tatu: Teknolojia, Watu, na Jamii.

.Teknolojia

Katika ulimwengu wa magharibi sisi mara nyingi tunakabiliwa na mtazamo wa ulimwengu unaoendelea ambao umewasilishwa na sekta ya vyombo vya habari na maendeleo katika kipindi cha miaka 60 isiyo ya kawaida – picha ya watu masikini ambao tu maisha yao ni ukulima mdogomdogo, kusafiri maili nyingi kwa siku kukusanya maji. Itakuwa sio sahihi kudai kwamba upatikanaji wa kilimo bora na maji safi bado si suala katika mabara kama Afrika, ila tunaweza kudai kuwa picha haiwakilishi Afrika yote.

Nchi nyingi Afrika zimeunganishwa sana, na Tanzania sio tofauti. Uunganisho huu unaruhusu fursa nyingi, ikiwa ni pamoja na shughuli za ramani za digitali zilizofanywa na wanaojitolea na wafanyakazi wa HOT. Aidha, wanachama wote wa timu ambao tumekutana hadi sasa ni Watanzania, kuonyesha kwamba njia ya jadi ya kutumia wataalamu kutoka nchi za Magharibi ni gharama zisizohitajika. Wakiwa na ujuzi wa ndani, watu hawa wanaojitolea wana uwezo wa wa kufanya kazi kubwa kwa muda mdogo na wanaweza kukusanya taarifa sahihi zaidi kutokana na lugha ya ndani na ufahamu wa kitamaduni.

Ramani Huria 2.0 imeona kuboresha ubora wa taarifa na mbinu zaidi ya usimamizi wa timu. Wasimamizi wa kazi wana nia ya kuongoza timu zao kwa mfano ili waweze kuonyesha michakato mzuri ya kukusanya taarifa, kuwahamasisha washiriki kufurahia kazi zao, na kuwasaidia kuona umuhimu wa kukusanya taarifa ya uhakika na sahihi. Teknolojia na mafunzo yaliyotolewa kwa timu, pamoja na kujitoa kwao na shauku ya ramani, kumewafanya kuwa moja ya timu zenye ujuzi wa ufanisi zaidi na wenye vipaji.

Mkutano wa Hali ya Ramani Tanzania 2017 ulioandaliwa na ramani huria na wadau uliohudhuriwa na washiriki 170.

Ramani ya Mitaro kata ya Mikocheni.

Watu

Wengi wanaojitolea ni wahitimu kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi wenye ujuzi unaohusiana ambao wanashiriki katika Ramani Huria ili kuboresha ujuzi wao wa kiufundi na usimamizi wakati wanachangia kuboresha jamii yao. Ramani Huria inatoa fursa kwa wanafunzi ya kujifunza aina mpya za ramani kama vile kutumia JOSM na QGIS, pia thamani ya kutumia wanajamii katika ramani.

Ramani Huria imegawanywa katika timu maalum kama, timu ya mifereji, Miundombinu, Ufikiaji wa jamii nk, kuruhusu wanaojitolea kujenga ujuzi wa kitaalam. Sehemu za mradi umegawanywa katika timu ya kukagua taarifa na timu ya kukusanya taariafa za ramani, na wasimamizi ambao huratibu kati ya vikundi ili kuhakikisha kuwa taarifa zilizokusanywa ni sahihi. Ukizungumza na timu, wengi wao hawajawahi kujua ramani ya jamii kabla. Sasa wanahisi kuwa wanaweza kurudi kwenye jamii zao wakati wakiongeza jumuiya kubwa ya ramani ya wazi. Ni msukumo kuona kwamba baada ya miaka mingi juu ya njia za maendeleo za kimataifa, sasa ni watu wa ndani ambao wanajiweka wenyewe kwenye ramani.

Washiriki wa mkutano wa Hali ya Ramani Tanzania

Jamii

Bado kuna njia ndefu ya kwenda katika mafunzo kwa jamii ili kuelewa jinsi ya kutumia ramani. Hata hivyo, kutokana na kile timu inasema, jamii zinaonekana kupokea wakati timu za kutengeneza ramani zinaelezea kile wanachokifanya wakati wa kupima mifumo ya maji ya mjini. Timu za ramani zinafanya kazi kwa bidii ili kusaidia watu wa ndani kuelewa dhana ya nyuma ya miradi na jinsi ramani zinaweza kuboresha mipango ya maendeleo na mipango ya dharura. Maono ni kuwa ramani zitumiwe na kila kiongozi wa kata na mtaa kuusaidia jamii yao ili watu waweze kujua maeneo yao wenyewe na huduma wanazohitaji kama; vituo vya afya, shule, vituo vya basi.

Timu ya kukusanya taarifa wakipima mtaro na kufanya kazi na wanajamii

Muhtasari wa Mawazo ya awali

Wakati msukumo wa awali wa mradi wa Ramani Huria ulikuwa ni kuboresha ujasiri wa mafuriko Dar es Salaam, ni wazi kwamba kuna faida nyingine za mradi huo. Mradi huu unasaidia watu wenyeji ambao wanahusika katika ramani, pamoja na kujenga jumuiya ya ramani. Njia ambazo miradi inafanya kazi inahimiza ushirikiano na jamii, ambayo ni njia ya kufurahisha ya kuendesha mradi endelevu.

Categories
Uncategorized

Ramani za Mitaro kwa Ajili ya Kutengeneza Kielelezo Maalum cha Mafuriko

Ramani Huria 2.0 inakusanya taarifa za mitaro kwenye maeneo yaliyo katika hatari ya mafuriko Dar es Salaam. Taarifa hizi zinatumika kutengeneza programu/kielelezo maalum cha mafuriko (flood model) ambayo inahitaji taarifa za mitaro zilizokusanywa kwa usahihi kama urefu, upana, kama mtaro umeziba (kwa majani au vitu vingine), muunganiko na kipenyo (Kwenye kalavati). 

Kutengeneza programu hii, Ramani Huria inafanya kazi na mtaalamu wa hydrolojia huko Deltares– Uholanzi, Hessel Winsemius. Dr. Hessel ni mtaalamu katika uwanja wa hydrolojia, hasa kwenye masuala ya kutengeneza vielelezo vya hatari ya mafuriko kikanda na kimataifa. Wiki hii alikuwa Dar es Salaam, kuangalia suala hili kwa ukaribu zaidi na timu yetu. Moja ya masuala makuu aliyoona ni ugumu ambao timu ilikuwa inapata katika kuhakiki ubora wa taaarifa- ilibidi kutambua makosa, taarifa zilizokosekana na taarifa zinazohitaji marekebishi kwa kienyeji kwenye programu ya QGIS kwa kuangalia sifa za mtaro husika. Hii inachukua mda mrefu na inachosha. Kwa usahihi, hakuna sehemu katika QGIS ambacho inashughulikia mahususi kwenye kuunganishwa kwa mifereji ya maji, hivyo Hessel aliunda programu (Python) lililoitwa Hydro-OSM  kufanya hivyo tu!

Drain Data Check Model

Ili kuhakiki ubora wa taarifa kwa ufanisi zaidi,  Hessel aliunda programu ya Hydro-OSM kwa ajili ya kuangalia ubora na ufanisi wa taarifa. Njia hii inafanya kusafisha taarifa kuwa rahisi zaidi kuliko njia iliyofanyika hapo awali, na hususani inaangalia sifa zinazofaa kwenye mifereji ya mjini. Kwa sehemu zenye makosa au kukosa taariafa, timu itarudi tena kwenye eneo husika kukusanya au kuhakiki taarifa hizo.

Hessel anaamini kuwa kama tukifanikiwa kutengeneza programu hii ya kielelezo cha mafuriko, itakuwa ni mwanzo mzuuri kwa wafanya maamuzi katika jitihada zao za kujenga jiji linalostahimili mafuriko. Pia anatarajia kusaidia wanajamii kutengeneza programu hii ya mafuriko.

Hessel akiangalia ufanyaji kazi wa programu

Lengo la haya yote ni kutumia taarifa za OSM kutengeneza programu ili kulinganishamtiririko wa maji kutoka eneo moja hadi lingine kwenye mtandao kama mitaro na mito nk.

Ili program kufanya kazi, mitaro inatakiwa kuungana zaidi iwezekanavyo. Ingawa baadhi ya mitaro/mifereji Dar es Salaam haijaungana, hessel anaendelea kulifanyia kazi suala hili ili kuona jinsi ya kuweka mitaro ambayo haijaungana kwenye programu.

Taarifa zote hizi zinahitaji muundo kamili wa programu ya ukusanyaji taarifa ambayo Ramani Huria imeshafanikiwa kutengeneza. Zaidi kuhusu programu hiyo ya mifereji ambayo imeundwa unaweza kusoma kwenye blogu iliyopita hapa

Categories
Uncategorized

Mkutano wa Hali ya Ramani Tanzania- 2017

Tarehe 8 hadi 10 Disemba Croud2Map na Ramani Huria walishirikiana kuandaa mkutano wa kwanza wa hali ya ramani uliofanyika Dar es Salaam, Tanzania. Mwanzoni tulitegemea washiriki 150 lakini watu waliofika walizidi makadirio yetu ya mwanzo na kufikia watu 170 kutoka nchi saba:  Malawi, Kenya, Uganda, Rwanda, Zambia, Ujerumani na Tanzania yenyewe. Ilikuwa tukio ambalo liliwaleta pamoja watu wenye taaluma tofauti tofauti kufanya mafunzo, kufahamiana na kushirikiana

Washiriki;

Mafanikio makubwa ya mkutano yalitokana na washiriki kuwa na taaluma tofauti tofauti. Waliohudhuria walikuwa watu kutoka Vyuo vikuu, Vijana watengeneza ramani, wanajamii, watafiti, viongozi wa serikali, idara ya ofisi ya raisi ya Marekani (Programu ya PEPFAR), Mashirika mbalimbali yenye nia ya kutumia ramani kutatua changamoto mbalimbali, wataalam wa compyuta na wafanyakazi wa  HOT. Washiriki hawa wote walitamani sana kujifunza kutoka kwa kila mmoja, kushirikiana na kuelewa jinsi ramani inaweza kuwa sehemu muhimu ya shughuli zao za kila siku.

uwasilishaji.

Timu ya Ramani Huria ilifanya kazi kubwa kuandaa mkutano, na vijana watengeneza ramani kutoka maeneo mbalimbali walikuwa na nia ya kusaidia watu wapya kwenye utengenezaji wa ramani. Ilikuwa ni vizuri kuona mmoja wa vijana kutoka Uganda kufanya mafunzo kwa washiriki kuhusu jinsi ya kutumia JOSM na Id- Editor katika kutengeneza ramani.

Mawasilisho mafupi

Kulikuwa na mfululizo wa mawasilisho ili kuonyesha kwa nini ramani ni muhimu na jinsi zinavyosaidia katika nchi nyingi na miradi. Kulikuwa na uwasilishaji kutoka kwa PEPFAR kuelezea jinsi ramani inavyosaidia kwenye mpango wao wa kuondokana na VVU / UKIMWI. Ramani Huria ilizungumzia kuhusu mradi wao unaoendelea wa ramani kwenye maeneo yenye hatari zaidi ya mafuriko na jinsi ramani zitatumika kwa ajili ya ustahimili na uamuzi. Map Kibera kutoka Kenya aliwasilisha jinsi ramani inavyosaidia katika utoaji wa huduma za kijamii kama usalama, usafi wa mazingira, afya na elimu. Mkurugenzi Mtendaji wa Mkoa wa Kigoma alielezea mpango wa WASH (Maji na Usafi) na jinsi ramani inavyosaidia katika utoaji wa huduma za jamii Kigoma. Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Heidelberg nchini Ujerumani ambao walishiriki katika kutengeneza programu ya Mapswipe pia walitoa maelezo mafupi juu ya jinsi programu hii inatengeneza ramani kwa urahisi.

Uwasilishaji- Ramani Huria

Meneja wa Nchi- HOT Tanzania Mr Ivan Gayton  alitoa maongezi mafupi juu ya mradi wa Mini-Gridi ambao una lengo la kutengeneza ramani za vjiji vinavyoweza kuwekewa umeme kwa kutumia paneli za nguvu za jua. Mradi huu una lengo la kutengeneza ramani za vijiji ambavyo bado havina umeme na kusaidia kutambua sehemu zinazofaa kwa mini-grids za nishati mbadala. Ramani hizi zinaweza kusaidia waendeshaji wa nishati ya jua kufanya haraka ili kutoa umeme mbadala kwa watanzania zaidi. Hii ni nguvu ya nini ramani zinaweza kufanya!

Baada ya mazungumzo hayo kulikuwa na majadiliano kati ya vijana mbalimbali wanaojihusisha na utengenezaji wa ramani, kujadili kuhusu uzoefu wao na nini wafanye kama vijana.

Majadiliano

Mapathon

Mapathon ni tukio linaloratibiwa kwa ajili ya kutengeneza ramani. Watu wanakaribishwa kufanya maboresho ya ramani kwenye eneo na kusaidia kufanya tathmini ya majanga. Mapathon hutumia tovuti ya mtandao kuhifadhi taarifa za ramani, yaani OpenStreetMap. Wakati wa mkutano tuliandaa Mapathon ya kutengeneza ramani ya Wilaya Manyoni- Kazi iliyoundwa kwa ajili ya kutengeneza ramani za ukeketaji wa wanawake. Washiriki walielekezwa kuhusu OSM Tasking Manager  na mafunzo jinsi ya kutumia programu ya  Id Editor  na  JOSM katika utengenezaji wa ramani.

Mapathon

Utangulizi wa QGIS,Map Swipe na Maps.Me

Washiriki walipewa utangulizi juu ya programu ya wazi na bure ambayo hutumiwa kwenye ramani. Watu walikuwa na nia sana ya kujifunza kuhusu QGIS, lakini siku moja ya mafunzo haitoshi kuweza kutengeneza ramani katika QGIS. Ambacho tuliweza kufanya, na ambacho kilikuwa na mafanikio mazuri, ilikuwa ni kuweka programu ya programu ya QGIS kwenye copyuta za washiriki, na kuhakikisha kuwa wote wanajua jinsi ya kuongeza shapefiles na data zinazotumiwa kufanya ramani.

Wakati wa mafunzo ya QGIS kulikuwa na maonyesho mafupi kuhusiana na drone na mpango wa kutengeneza ramani za vijiji vya Tanzania kwa kutumia drones. Dhana ilitolewa vizuri sana na Mr Ivan Gayton ambapo alionyesha haja halisi ya drone kusaidia na maandalizi ya dharura. Kuwa na mzunguko kamili na ufanisi wa majibu unahitaji ramani na eneo lenye vifaa. Ili kujenga ramani hizi unahitaji kukusanya taarifa kutoka kwa jamii kulingana na picha zitakazotumiwa kwa kukusanya taarifa. Ili kuwa na picha unahitaji drone ambayo husaidia kukamilisha mzunguko kwa kutupa picha nzuri ya kukusanya taarifa na hivyo jamii hizi zinaweza kupata msaada bora.

Picha ya Pamoja.

.

Mwishoni mwa Mkutano tulikuwa na mechi ya soka- OSM Tanzania VS Watu wengine, na OSM Tanzania ilishinda mechi.

Ilikuwa tukio la kuvutia sana na la mafanikio. Waandishi wa habari walikuwepo na mkutano wetu pia ulionyeshwa katika moja ya televisheni maarufu nchini Tanzania- International Television network-Tanzania (ITV), kituo cha Kimataifa cha China Global Television Network (CGTN) and Daily news paper

Kwa ujumla, ilikuwa uzoefu mkubwa kwetu kama waandaaji na pia kwa washiriki. Tayari tunatarajia mkutano wa pili wa hali ya ramani Tanzania mwaka 2018!

Categories
Uncategorized

Ramani Kwa Ajili ya Siku ya VVU / UKIMWI Duniani- 2017

Katika heshima ya Siku ya UKIMWI Duniani 2017, Ramani Huria na Tanzania Data Lab (dLab) waliandaa tukio kuongeza ufumbuzi kwa njia ya uwazi, uwajibikaji na ushirikiano. Lengo ilikuwa watu kujifunza jinsi ramani inavoweza kuongeza uhuru na upatikanaji wa habari kwa umma juu ya VVU / UKIMWI katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Tuliamua kutengeneza ramani ya Geita wilaya iliyopo katika ukanda wa ziwa Victoria ambapo wilaya hii ni moja ya wilaya zinazongoza kwa ukatili wa kijinsia kutokana ukatili huu watu wamepata ulemavu wa moja kwa moja uliosababishwa na ukatili huo. Ni wazi kuwa maeneo ambayo yana ukatili wa kijinsia pia huwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya VVU / UKIMWI.

 Utengenezaji wa ramani ukiendelea

Katika tukio hilo, watu wa kujitolea walipata utangulizi wa  kwa nini sisi hufanya matukio ya kutengeneza ramani, na jinsi ambavyo tunaleta pamoja waandaaji ramani, wafanyakazi wa kujitolea na jamaa wengine katika uwanja wa kujifunza jinsi ya kuingiza taarifa kwenye OpenStreetMap, kutengeneza ramani za bure/huru na zinazopatikana kwa urahisi kwa ajili ya matumizi ndani ya nchi na ya kimataifa – kwa upande wetu lengo lilikuwa juu ya VVU / UKIMWI.

Washiriki wetu walipata utangulizi juu ya mradi wa Ramani Huria. Walijifunza jinsi ramani husaidia jamii, na jinsi tukio hili linaweza kusaidia kuzalisha taarifa kwa ajili ya watu Geita.

Kabla ya kuanza kuchora ramani, tulihakikisha kwamba kila mtu alikuwa na;

  • Laptop, MacBook, au Desktop.
  • Kipanya (kufanya uchoraji kuwa  rahisi)
  • OSM akaunti (mtu anapaswa kuwa nayo ili kuweza kuingiza taarifa kwenye OSM).
  • Mtandao.

Waliohudhuria walipewa mafunzo ya jinsi OSM inavyofanya kazi, na jinsi ya kuingiza taarifa kwa kutumia JOSM na Id Editor. Baada ya hapo walielekezwa kuhusu  OSM Tasking Manager. Hichi ni chombo cha ramani  kilichoundwa na kujengwa kwa ajili ya watengeneza ramani. Madhumuni ya chombo ni ya kugawanya eneo katika sehemu ndogo ndogo ambazo zinaweza kukamilika kwa urahisi. Chombo hichi  kinaonyesha maeneo ambayo bado yana unahitaji wa kuchora ramani na ambayo yamemalizika ila yana haja ya kuthibitishwa.

Washiriki walianza kutengeneza ramani, wakichora barabara na majengo na baadae kupakia kwenye mtandao.

Kufanya tukio kuwa shirikishi na la kuvutia, tuliofanya michezo kama vile OSM fights. Mchezo huu unakuwezesha kuingiza majina ya watumiaji wawili unaaanza mpambano wa kufurahisha kati majina ya watumiaji wawili kulingana na ‘Jinsi gani mtu kachangia kwenye OSM’. Na mwishowe mshindi ataonekana.

Kutangaza mshindi kila baada ya kila dakika 30 kulileta motisha kwa washiriki kuendelea kuchora ramani kwa kasi. Bila shaka, kila mtu angekuwa na furaha kuona kuwa ni mshindi, hivyo hii ilileta ushindani mkubwa kwa washiriki.

Picha ya pamoja ya washiriki

Tukio lilikuwa  na mafanikio halisi na watu walikuwa na nia ya kujua wakati mwingine wa  kufanya mapathon ili waweze kushiriki tena. Ni fahari yetu kuona jinsi jamii yetu ya watengeneza ramani inakua siku hadi siku.

Categories
Uncategorized

Kujenga Zana za Wazi kwa Ajili ya Kutengeneza Ramani za Mifereji

Lengo la Ramani Huria ni ustahimilifu: Kupunguza athari za mafuriko kwa binadamu. Njia ya kawaida kabisa ya kupunguza hili ni ni kuondoa uwezekano wa mafuriko! Mifereji ni moja ya njia ya kufanya hili.

IMG_1483.JPG
IMG_1492.JPG

Culvert                                                          Concrete Drain

ff40e47d-920f-441f-9bad-399dd3d5dd70.jpg
silt.jpg

Ditch                                                                             Silt Trap  

Mfumo wa mifereji ya maji  Dar es Salaam ni mkubwa na mgumu, mamia na maelfu ya mifereji mara nyingi kando ya barabara, Mara nyingi zinaanzia urefu wa mita tatu mifereji ya kujengwa pembeni ya barabara hadi sentimeter tano za mifereje iliyochimbwa na watu wenyewe kutoka kwenye makazi yao. Kusaidia kupunguza mafuriko, tunaweza kutengeneza ramani za mifereji na kuchambua katika programu maalumu ya ufanisi wa hydrolojia. Hii inaweza kutusaidia kujua tatizo na sehemu ambayo inahitaji marekebisho, kuundwa upya au kusafishwa tu na wana jamii. Ili kuchambua mifereji ya maji, tunahitaji zaidi ya mistari kwenye ramani. Tunahitaji wasifu (Sura), vipimo, urefu, aina ya vifaa, na mwonekano wa mfereji. Hata hivyo programu hii ya hydrolojia inahitaji kila kipande cha mfereji kwenye ramani kiunganike, kisikosekane kitu na chochote kisikae vibaya (Kila kitu kikae kwenye sehemu yake ili kuwezesha programu hii kufanya kazi)

Aina hii ya ramani imekwisha kuwa kuhifadhiwa na watafiti wenye ujuzi sana kwa kutumia vifaa vya gharama kubwa. Hata hivyo Ramani Huria imeona fursa ya kufanya kazi na wanafunzi wenye uwezo mkubwa kutoka chuo kikuu cha Ardhi pamoja na wana jamii wenye uelewa wa maeneo yao wanayoishi. Muunganiko huu umesababisha ukusanyaji wa taarifa kwa kiwango kikubwa, na kujikita sehemu nyingi zinazokumbwa na mafuriko Dar es Salaam.

IMG_2386.JPG
IMG_1021.JPG

        PICTURE: Measuring Sticks and Tapes, Showing Hinge on Measuring Sticks.

Kwanza tulianza kwa kuunda fimbo maalum, ili kupata vipimo vya mifereji kwa usahihi (Kwa hakika bila kutumia muda mrefu kuvitengeneza) na kununua tape (futi). Hata hivyo, Licha ya kuwa simu zetu zinapokea GPS, Hatukujua programu yenye suluhisho ambayo ingeturuhusu sisi kuchukua mistari kwa usahihi iwezekanavyo, pamoja na kuchukua vipimo mbalimbali kwenye muundo uliopangiliwa.

Programu tulizopata zilikuwa kwenye makundi mawili;

  • Programu zinazo jikita kwenye kurekodi mistari ya GPS, na
  • Programu zinazo jikita kwenye kuingiza taarifa.
Screenshot_2017-10-26-15-27-19[1].png

                      SCREENSHOTS: Various Android Mapping Applications

Hatukupata chochote ambacho kiliweza kufanya haya yote kwa usahihi. Programu nyingi za Android zinamruhusu mtumiaji kukusanya kiwango kikubwa cha taarifa za mistari ya GPS zenye ubora (Ndani ya kiwango cha ubora wa GPS), ikiwepo ramani inayoonyesha sehemu mtu alipo, uwezo wa kuimarisha ikiwa mstari unapoteza usahihi sehemu moja kwa moja, na uwezo wa kuchuja pointi ambazo hazijakidhi  vigezo sahihi.

data.JPG
dataww.JPG

SCREENSHOTS: OpenDataKit with Various Data Types

Programu nyingine, Hasa OpenDataKit (ODK) ambayo tunaitumia kwa kiango kikubwa wakati wa kuchukua taarifa, inamruhusu mtumiaji kujaza aina maalum ya fomu. Form ya ODK inaweza kuchukua namba ( tarakimu au desimali), maandishi, chaguo kutoka kwenye orodha (chaguo moja au “radio button”, au chaguo nyingi kwa kuchagua kila kinachotumika) na hata picha kutoka kwenye kamera ya simu. Hata hivyo kipengele cha GPS cha kuchukua mistari inapingwa na kuchukua mstari mmoja, haikujitosheleza kabisa. Pale ambapo GPS haikupata satelite , ODK itaanza kutumia pointi ya eneo la mtandao (iliyokokotolewa kutoka kwenye minara ya simu iliyokaribu) ambayo iko mbali kwa mamia au hata maelfu ya mita ( hii ilisababisha mistari iliyochorwa kuruka mbali na haikuweza kutumika kutengenezea ramani).matatizo mengine yalihusisha kutokuwa na uwezo wa kuchagua kizingiti/sehemu kwa usahihi, huwezi kufuta labda pointi chache za mwisho (inakubidi uanze upya pale ambapo kitu hakipo sawa), hakuna njia ya kuonyesha kwa karibu sehemu ambayo mtu yupo,  na muundo wa matokeo ambao haukuwa na upeo na taarifa ya usahihi (zote zinapatikana kutoka kwenye mpangilio wa GPS).

Uchaguzi wetu ulikuwa:

  1. Kutumia programu ya ramani kama vile ya OSMAnd,  ya bure na ya wazi kabisa,na kurekodi taarifa yote katika sehemu  moja ya “maoni”. Hii itahitaji mafunzo na usimamizi mkubwa ili kuhakikisha kuwa taarifa zote zinakusanywa kwa mtindo thabiti.
  2. Kutumia programu ya kuingiza taarifa kama ya ODK yenye uwezo mdogo wa kuchukua mistari, na kuzingatia mapungufu yake.Hii ingeweza kusababisha wachunguzi kutumia muda mwingi kuchukua kila mstari kutokana na kulazimishwa kurudia tena, na utaweza kusababisha matokeo mabovu ya mstari mzima.
  3. Kutumia programu  moja kurekodi mistari, na nyingine kuingiza taarifa, hii itahitaji uhifadhi makini ili kuhakikisha kuwa taarifa zimeingizwa kwenye kwenye mstari sahihi. Wakati wowote taarifa na mistari zikiwa nje ya utaratibu, basi seti nzima ya taarifa itakuwa haina matumizi na itabidi ikusanywe tena (uwezekano wa siku au wiki nyingine za kazi)
  4. Kutengeneza programu ambayo ni bora kwenye kuchukua taarifa au programu ambayo ni nzuri kwenye kuuingiza taarifa za ramani.

Akaingia Ka-Ping Yee, Mhandisi wa programu mwenye ujuzi wa ajabu mwenyenia kubwa ya kufanya kazi za kibinadamu. Ping alikuwa likizo uingereza wakati tunampigia kumuomba msaada, na alikubali kukaa siku chache Dar ea Salaam akijitolea kufanya kazi na Ramani Huria. Tulitaka kazi yetu imsaidie yeyote kwenye ulimwengu wa kutengeneza ramani za kibinadamu/kijamii, na hivyo tunapendelea kwa kiasi kukubwa kutumia programu huru na za wazi kabisa.

Kwa haraka tulianza mkakati wa kuongezea ubora programu huru ya OpenDataKit (ODK) ili iwe na uwezo wa kuchukua mistari kwa usahihi. ODK kwa miaka mingi imekuwa rasilimali kubwa kwenye miradi ya kidigitali ya kibinadamu, hasa kwa sababu ya uwazi na kujitolea kwa jumuia ya watengenezajiwa programu hii. Tulijua kwamba, ikiwa tutaongeza kazi kwenye ODK, si tu Ramani  Huria ingeweza kufaidika, lakini sekta nzima ya kibinadamu ingeweza kufaidika maboresho yetu.

Kuchangia kwenye programu programu huru /wazi ni ngumu zaidi ya inavyoonekana. Kabla ya kufanya marekebisho kwenye mradi, ni muhimu kuwasiliana na jamii ambayo imeunda na inaendeleza programu hiyo. Kama hili halitafanyika, ni rahiisi sana kurudia kazi ambayo tayari ilishafanyika au hata kufanya marekebisho ambayo  hayatapatana na kuvunja/kuharibu sehemu nyingine za programu. Kwa sababu hiyo, wakati mwingine watengenezaji wa programu za wazi wanakuwa na hisia kali na miradi waliyotengeneza, na wanaweza kujitetea/kujilinda endapo mtu ataingilia mtoto(programu) ambaye wamekuwa wakimpa upendo, muda, na uangalizi, hasa kama wageni wataingia bila kujitambulisha na kuonyesha unyenyekevu kidogo. Zaidi ya hayo, mabadiliko ya programu hayapaswi kufanywa yote kwa mara moja, bali kwa kuingiza mabadiliko kwa kuyatenga, ikihusisha na nyaraka za wazi, kuruhusu kujaribiwa na kuhakikiwa ili isiharibu mambo. Mpangilio wetu wa maboresho ya kificho (code) ya Ping ulifikia mabadiliko kadhaa tofauti, na utahitaji ufungaji kama mtu binafsi (“kiungo”) (kiungo fulani na ufafanuzi wa vitendo vya git) pamoja na majadiliano na diplomasia.

Tuliwasiliana na Helen Martin, moja kati ya watengenezaji wa ODK, na jamii ya ODK kwa kiasi kikubwa walitukaribisha na walifurahushwa na kazi yetu. Ping ali “fork repo” ya ODK, na akaja Tanzania kuanza kazi.

Kulikuwa na matatizo machache makuu yaliyotaka kusababisha ODK karibu isiweze kuchukua taarifa za mistari. Kuruka mara kwa mara kwa point ya GPS kwa sababu ya mtandao, kutokuwa na uwezo wakuweka kizingiti kwa usahihi, na ulazima wa kuanza mwanzo wakati kitu chochote hakijaenda sawa ndio kubwa zaidi. Ping alianza kwa kuongeza usahihi wa kuchuja na kutengeneza button “backspace” kufuta point za mstari zilizochukuliwa mda huo.( kwa hiyo mtumiaji angeweza kurudi nyuma kwenye baadhi ya pointi na sio kuanza mwanzo).

spreadsheet.JPG

SCREENSHOT: The Prioritization Spreadsheet

Kila siku Ping aliwauliza Sadah na Felix, (Wanaotengeneza ramani za mitaro), Randy Jones (anayejitolea kutoka Canada) na Ivan Gayton (Meneja wa HOT-Tanzania), kuona ni mabadiliko gani yangeweza kusaidia kazi ya timu. Hii ilikuwa uwiano mkali kati ya mabadiliko ambayo yatakuwa na athari nyingi na yale ambayo yatachukua muda mwingi; “mafanikio ya haraka” (athari kubwa na rahisi kutekeleza) ilichosha kwa haraka.

Masuala machache yalitokea kuwa magumu zaidi ilivyodhaniwa. Kwa mfano ODK inahamisha mistari kama mmfululizo wa pointi ambazo hazielezwi na kitu chochote zaidi ya namba nne (Latitudo, Longitudo, Mwinuko  an usahihi wa GPS) uliotenganishwa na koma na mikato mwili katiya pointi). Programu za ramani hazijui nini cha kufanya juu ya mfululizo huu bila muktadha. Kwa hiyo tunabadilisha muundo kwenda kwenye nakala inayojulikana (well known text), mfumo wa taarifa za kijografia za programu za ramani kama QGIS, programu ya ramani ya bure na wazi tunayoitumia ambayo inaweza kutambua na kuonyesha taarifa hizi.

Capture.JPG

SCREENSHOT: Some WKT String Examples

Hata hivyo, tuligundua kuwa hii iliivunja/haribu ODK! Wakati wowote mtumiaji akijaribu kufungua  tena dodoso baada ya kulihifadhi, mistari ya nakala nakala inanyojulikana inapotea. Inabadilika kuwa lugha ya ufafanuzi wa fomu ambayo ODK imekataa, Javarosa ina sarufi maalum kwa ajili ya mistari – mfululizo uliotajwa hapo juu wa namba nne zilizoteuliwa na koma mbili kati ya pointi – ambazo haziendani na Well Known Text (au muundo wowote wa kijiografia ambao tunajua). Bila kufanya marekebisho makubwa kwenye Javarosa (ambayo kwa kweli ingevunja mambo mengine,  hasa kwa watu wa mbali ambao hawawezi kujua nini tumefanya, na wangetuchukia wakijua tulichofanya), hatukuweza kutekeleza vifungo vya nakala zinazojulikana viizuri katika ODK. Tulipaswa “kurekebisha mabadiliko” na kurudi kwenye utekelezaji wa awali ambao hutoa taarifa ambazo haziwezi kufunguliwa katika programu ya ramani. Kutatua, au angalau kupunguza hii Ping aliandika [Plugin utility plugin] (github.com/zestyping/THE LINESTRING PLUGIN) kwa QGIS kubadili mistari ya Javarosa katika nakala inayojulikana vizuri.

Screenshot_2017-10-26-15-40-57.png

SCREENSHOT: The New ODK Line Trace Interface

Mabadiiliko mengi ya kiufundi baadae, tuliishia kujadili kitu kingine kipya kabisa: Wataalam wa ramani pale chuo cha Ardhi walivyojaribu kuangalia taarifa walizokusanya kwenye compyuta waligundua kuna baadhi ya pointi na vipande havionekani. Wataalam hawa , mbali na juhudi walizozifanya hasa Sadah, Randy na Feliix, baadhi ya taarifa zilikosekana, ilikuwa adimu, lakini taarifa za nyingi zilitumwa kwa mtaalamu wa hydrologia hazikukamilika na nyingine hazikuungana. Wasimamizi walishindwa kujua  kama taarifa zote zimechukuliwa, na walitakiwa kusubiri hadi wataalam wa ramani waangalie kwenye compyta wakiwa chuo. Tuliwaza ‘’Vipi kama wataalam na wasimamizi wanaweza kuona vipande vyote na pointi kwa mda sahihi, ili waweze kujua kitu gani hakijachukuliwa kabla ya kuondoka kwenye eneo. Kwa hiyo Ping alitengeneza kitu kingine, alitengeneza portal kwenye mtandao ambayo ingemwezesha msimamizi wa ramani kuona pointi na mistari kwenye mtandao (simu au compyuta) kabla ya kuondoka kwenye eneo la kukusanya taarifa.

Kobo view.JPG
Screenshot_2017-10-26-15-44-48.png

            SCREENSHOTS:     Kobo Viewer on Laptop            Kobo Viewer on Phone

Hatimaye, tuna suluhisho la programu yenye uwezo wa kuchukua mistari ya GPS kwa kiwango cha usahihi na ufanisi tunaohitaji, uwezo wa ajabu wa ODK kuingiza aina sahihi za taarifa, na chombo cha usimamizi  cha kusimamia timu kukamilisha kikamilifu kazi ya ukusanyaji taarifa za ramani. Hata hivyo bado sio mda wa kusherehekea, bado kuna vitu vingi vya kufanya.

“Fork” na mabadiliko yetu yote kwenye ODK bado haijaunganishwa kwenye “codebase” kuu ya ODK (majadiliano na jamii ya ODK inaendelea, na kazi zaidi inapaswa kufanyika kwenye nyaraka na ufungaji). Tumetengeneza ramani saba za Dar es Salaam kwa kutumia njia zetu, lakini sehemu ndogo tu ya ramani imethibitishwa na wataalam wa programu ya hydrologia nchini Uholanzi; tunahitaji kuhakikisha kuwa kazi yetu inafaa kikamilifu kabla ya kuanza kutengeneza ramani za mji wote. Mwishoni, tunahitaji kuandika kazi yetu yote, kuifunga, na kuandaa kitabu kwa  mtu mwingine yeyote ulimwenguni ambaye anaweza kuboresha mifereji ya mijini kupitia ramani za jamii!

Kipindi Ping anafanyia kazi programu, Randy Jones, aliyejitolea kutoka Canada kuongoza timu ya wanaotengeneza ramani za mifereji mwezi wa mwanzoni, anatengeneza  Wiki-based playbook for practical community-based urban drainage mapping  kulingana na njia ambazo tumeanzisha Dar es Salaam na Ramani Huria. Tunatarajia kazi ya Ramani Huria itafaidisha idadi kubwa ya watu ulimwenguni kote walio kwenye hatari ya mafuriko. Timu yetu hapa hapa Tanzania itaongoza njia!

Categories
Uncategorized

Uzinduzi wa Ramani Huria 2.0

Tarehe 26 Septemba 2017, ukurasa mpya wa RAmani Huria 2.0 ulifunguliwa rasmi kwenye ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Tukio lilihudhuriwa na wadau muhimu wakiwemo maafisa wa serikali, maafisa wa vyuo vikuu, Washiriki kutoka kikosi  cha msalaba mwekundu, wataalamu wa ramani, wana jamii, na bila shaka wanafunzi wa Ramani Huria. 

Profesa Evaristo Liwa, Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Ardhi, alitoa neno la ufunguzi akianza kwa kueleza kazi iliyopita ya Ramani Huria – Mradi ambao ulifanikiwa kutengneza ramani za kata 21 katika jiji, makazi ya takribani watu milioni 1.3. Alibainisha kuwa awamu hii iliyopanuliwa inatarajiwa kufikia makazi ya zaidi ya watu  milioni tatu wa Dar es Salaam, Mara mbili ya mradi wa mwanzo wa majaribio

Risala ya Profesa Liwa ilijikita kwenye umuhimu wa ushirikiano kwenye mradi huu – akionyesha ushirikano kati ya chuo kikuu cha  Ardhi na benki ya dunia ambao hadi sasa wameweza kuhamisha ujuzi na maarifa ya usimamizi wa athari za maafa kwa wanafunzi zaidi ya mia nne. ‘’Kupitia msaada kutoka benki ya dunia na mradi wa Ramani Huria, wahitimu wengi wa Chuo Kikuu cha Ardhi wamekuwa wataalamu na kuajiriwa katika sekta mbalimbali,” alisema.

IMG_1823.JPG

 Profesa Evaristo Liwa- Makamu mkuu wa chuo kikuu cha Ardhi akifungua warsha

Bwana Michael Ole-Mungaya, mwakilishi wa katibu tawala mkoa-Dar es Salaam alifuata kuupa sifa mradi, sasa Ramani Huria ni kampeini kubwa ya ramani za jamii duniani. Alianza kwa kubainisha kuwa Dar es Salaam ni jiji linalokua kwa kasi na ongezeko la tatizo la ukusanyaji taka, moja kati ya vitu vinavyochangia mafuriko. Kufuatia hili, alisisitiza kwamba msaada kwa Ramani Huria unaendelea kutoka pande zote, kwa njia ya ushirikiano huo tunaweza kufanya mji wetu kuwa na nguvu zaidi.

Mkurugenzi wa benki ya dunia – Tanzania, Bi Bella Bird, alitukumbusha zaidi kwamba Tanzania ni waathiriwa zaidi wa mafuriko Afrika Mashariki, na kwamba mzigo huu unaongezwa sana na idadi ya watu kutoka kwa mtazamo wa kijamii na kiuchumi. Alisisitiza umuhimu wa kupanua mradi kama Ramani Huria na alikuwa na furaha kuripoti kwamba Benki ya Dunia haitacha msaada wake.

Picha ya pamoja ya washiriki

“Nini sababu ya mpango Ramani Huria kuwa wa kipekee” Thomas Allen Naibu Mkuu wa Idara ya  Maendeleo ya Kimataifa – Uingereza (DfID), aliendelea “Ni vijana na ubunifu” Kama alivyoongea Bi Bella , bwana Allen aliongeza kuwa Uingereza inafurahia kuunga mkono mpango huu katika lengo lake kuu la kuboresha ustahimilifu wa miji nchini kote.

Mwishoni mwa warsha, Mkataba wa makubaliano ulisainiwa kati ya chuo kikuu cha Ardhi, benki ya dunia na DfID kama makubaliano rasmi ya kuongeza ushirikiano kati ya wadau hawa na kuboresha upatikanaji wa elimu ya vitendo kwa vijana juu ya usimamizi wa athari za maafa 

Kutia sahihi mkataba wa makubaliano

Baada ya picha za pamoja za kusherehekea, washiriki walikaribishwa kwenye maonyesho ya kazi ambayo Ramani Huria imekuwa ikifanya hadi sasa – ambazo ni kutengeneza ramani za mifereji, ramani za kiwango cha mafuriko, ramani za miundombinu, na hatua za dharura.

IMG_1904.JPG

Maonyesho

Categories
Uncategorized

Kuwafikia Wanajamii kwa Ajili ya Kutengeneza Ramani za Kiwango cha Mafuriko- Kata ya Hananasif

Moja ya kazi ya msingi ya Ramani Huria ni ku tathmini kiwango cha mafuriko Dar es Salaam -na ushiriki wa wanajamii ni kitovu cha shuhuli hii. Nikupitia ushiriki huu ndipo tumepata ujuzi wa ndani na kuongeza kwa kina kiwango cha kutambua maeneo hatarishi ambayo yanaweza kutolewa na jamiii yenyewe.

Kutumia taarifa zilizokusanywa, tuna uwezo wa kuunda mfululizo – kuendeleza uwezekano wa kutambua mwenendo wa kihistoria wa kiwango cha mafuriko jijini Dar es Salaam. Kupitia njia hii, tunaweza kuchunguza jinsi hali ya mafuriko ilivyobadilika mwaka hadi mwaka, na ushirikiano wa wanafunzi na wanajamii ni muhimu kwa uzalishaji wa taarifa na ustawi. Baadaye kukamilika kwa tafiti zitategemea muungano kati ya wana jamii na mradi huu.

Jinsi kazi ilivofanyika  

Baada ya kukutana na viongozi wa ngazi ya mtaa,wanafunzi wanaenda nyumba hadi nyumba kuelezea mradi kwa wanajamiii, kama mwananchi atavutiwa, basi mwanafunzi atamuonyesha jinsi ya kutumia programu ya Opendatakit Collect (ODK) na kuwaeleza jinsi ya kujaza utafiti kwa usahihi. Vocha za simu na motisha ya fedha hutolewa kwa wale wanaofanya uchunguzi, kama chanzo cha motisha kwa ushiriki wa jamii katika kufanya kazi na sisi.

Wana jamii wapya hupelekwa kwenye mto na wanafunzi na kuelekezwa jinsi ya kutumia programu. Kutoka pointi/sehemu waliyosimama kwenye mto, wanajamii wanaelekezwa kutembea moja kwa moja mbali na mto ili kuchunguza/kutafiti nyumba njiani – kutambua kama wanapata au laa. Mwanafunzi anaambatana na mwana jamii kwenye nyumba 1 au 2 na kisha anamuacha mwana jamii huyo kuendelea mwenyewe ili kukamilisha utafiti huo. Hii hutumiwa kama mbinu ya kukusanya taarifa wakati mtu anatembea. (transect-like data collection methodology).

ttttttttttttttttttttttttttttttttt.JPG

Mwanafunzi akimuelezea mwanajamii jinsi kazi inavfanyika

Mara baada ya mwana jamii kurudi, Mwanafunzi atasimamia mbadilishano wa maarifa kati ya wanajamii wenyewe. Mwanajamii aliyerudi sasa anakuwa mwalimu na kusaidia kuwaunganisha wananchi wengine kwenye shuhuli hii.

Changamoto

Shuhuli/kazi hii bila shaka ina baadhi ya changamoto. Kuligundulika mapema kuwa baadhi ya maswali ya utafiti yalifafanuliwa vibaya, kwa mfano.’umewahi kupatwa na mafuriko?’ Wanajamii wengine walijibu kupatwa na mafuriko kupitia anuani zilitopita( makazi mengine ambayo walikuwa wakiishi hapo kabla). Kuandika tena na kufafanua utafiti huu kwa baadhi ya wanajamii kulifanyika na wanafunzi waliendelea kufanya mafunzo zaidi.

Baadhi ya wana jamii wamekuwa wakisita kushirikiana kwa sababu ya kutoaminiana /kutokuwepo kutambuliwa kwa wachunguzi wanafunzi. Hili suala  tumelishughulikia kwa kutoa barua za utangulizi kuhusu mradi.

Wanajamii wengine wamehama  nyumba kwa sababu ya matukio ya mafuriko na , hivyo baadhi ya pointi za GPS haziwezi kuwekwa kama kumbukumbu za mafuriko. Inaweza kuwa zoezi la kuvutia kujua ni watu wangapi wamehama kutokana na mafuriko ili kuona jinsi gani mafuriko yameathiri idadi ya watu.

Matokeo

Licha ya changamoto hizi, namba ya tafiti zilizofikiwa ni zaidi ya tulivyodhani kuwa inawezekana. Ukuaji wa namba za utafiti umekuwa mkubwa sana – kuanzia tafiti mia moja tu kwa siku moja hadi zaidi ya 840  kwa siku moja, ukuaji uliofanyika ndani ya siku 8 tu. Hii sio tu inathibitisha jinsi ushiriki wa jamii unavyo zaa matunda , bali ni kwa kiasi gani tuna uhakika wa kusonga mbele. Mashaka yote ya awali juu ya lengo la mradi yamemalizwa na kupanda kwa takwimu hizi za uchunguzi, Hii inaonyesha kwamba kiwango kikubwa zaidi kitafikiwa. Hadi sasa, tuna tafiti zaidi ya 1000 zilizokamilika.

Kwa ongezeko la msaada kutoka kwa wanajamii, tuliwachukua wanajamii nane (kutoka Hananasif na Kawawa) kuja mtaa wa Mkunguni ‘A’ kuona jinsi gani tunashirikiana na viongozi wa mtaa. Kufuatia utaratibu uliowekwa na wanafunzi kwenye kata ya kwanza tuliyozuru, Wamajamii walishirikiana kikamilifu na viongozi wa mtaa, kuuliza kuhusu mipaka ya mtaa na kuuliza kuhusu eneo hilo.Pia tuliandaa kikao na wanajamii pamoja na viongozi wa mitaa, tunatambua kuwa kuimarisha uhusiano huu kutafanya mradi kuwa endelevu.

commmmmmmmmmmmmmmmmmm.png

Kikao na Viongozi wa Mitaa

Katika mchakato huu, Imegundulika kuwa mifereji mibovu na iliyoharibika kunachangia mafuriko kwa kiasi kikubwa kwenye maeneo yaliyopo mbali na mto. Sababu hizi zimegundulika kupitia wanafunzi kuwashirikisha wanajamii kikamilifu – baada ya kuangalia taarifa hizi na kuonyesha kwa pamoja sehemu ambazo si rahisi mafuriko kutokea. Hii ndiyo sababu kushughulikia mafuriko ni suala gumu sana ambalo linahitaji ushirikiano mkubwa kati ya watendaji husika, timu ya Ramani Huria ni kati yao.