Categories
Uncategorized

Sanaa ya Ramani za Mifereji ya Maji Dar es Salaam 

Moja ya malengo makubwa ya Ramani Huria 2.0 ni kuongeza juhudi zilizofanyika kwenye ramani za mifereji zilizofanyika wakati wa majaribio ya mradi. Wanafunzi sasa wamegawanywa katika makundi mbalimbali ili kurahisisha uratibu na kuwapanga kulingana na ujuzi.Makundi haya ni pamoja na; Timu ya mifereji, Timu ya GIS, Timu ya  Open map kit,Timu ya kuwafikia wana jamii,na timu ya kutengeneza ramani za mbali.(bila kuwa sehemu husika)

Hakukuwa na njia inayojulikana ya kutegeneza ramani za mifereji, Hivyo timu  yetu ilibidi kujaribu njia mbalimbali zinazofahamika za kutengeneza ramani, baada ya kujaribu, Kipengele cha Geotrace pamoja na uwezo wake wa kuwezesha utengenezwaji wa tafiti zilizoboreshwa, iliwekwa na ODK pamoja na programu zote zilizojaribiwa. Hii ni programu ya simu ya mkononi (Android) ya bure na ya wazi ambayo husaidia mashirika kukusanya taarifa na kusimamia ukusanyaji wa taarifa kwa kutumia simu ya mkononi. Form ya kukusanya taarifa hutengenezwa (XLS Forms inashauriwa kwa ukusanyaji wa taarifa nyingi) na ukusanyaji wa taarifa unafanyika kwenye simu ya mkononi. Kisha hutuwa kwenye seva ambayo inaunganisha taarifa na kufanya ipatikane kwenye mifumo mbalimbali kwa ajili ya matumizi.

Baada ya kutengeneza/kuunda fomu sahihi, Wanafunzi walifundishwa jinsi ya kutumia ODK kwenye simu zao.  OSMAnd ni programu nyingine inayowasaidia wanafunzi kuwa na mwelekeo sahihi wakati wanazunguka kutengeneza ramani jijini, Na kazi ya GeoTrace inasaidia sana kwa ramani ya mifereji na makalavati kwa kuchukua pointi kwa usahihi wakati mwanafunzi anachukua taarifa ya kitu husika.

.

Mwanafunzi akichora mtaro

Kwa kuongeza, Wakati wa kukusanya taarifa, wanafunzi wanatumia ODK kuchukua pointi kwa usahihi kando ya mfereji. Pointi hizi ni pamoja na mwanzo wa mfereji, Mfereji ulipoharibika au kufungwa, Sehemu ambayo mfereji unaungana na mali binafsi, Sehemu ambayo mfereji umeingia, Sehemu mfereji unapotoka na nyingine nyingi.  

Ili kupata vipimo sahihi vya taarifa mbalimbali za mitaro au makalavati, zana zinazofaa kwa kusudi hili zilihitakiwa. Ilihusisha vifaa kama utepe wa kupimia (Tape measure), kutumia fimbo iliyotengenezwa kwa vipimo (iliyoundwa na timu yetu ya tanzania) kupima urefu na upana wa mitaro pamoja kipenyo cha kalavati. Takwimu za mifereji ya maji zinahitajika kupimwa kwa usahihi kwa kuwa lengo la Ramani Huria ni kuboresha ustahimilivu wa mafuriko kwenye jiji, na mirereji ina mchango mkubwa katika hili.

IMG_1129.JPG

Wanafunzi wakipima kina cha mtaro kwa kutumia fimbo iliyotengenezwa kwa vipimo

Kwa majaribio ya uelewa wa wanafunzi katika mchakato huu wa kutengeneza ramani tuliwapeleka kata ya Hananasifu kwa ajili ya kukusanya taarifa. Wanafunzi walijigawa wenyewe katika makundi kulingana mitaa kisha wakatanwanyika kukusanya taarifa. Mchakato ulikua na changamoto kadhaa kwasababu ilikuwa ndo mara ya kwanza kwa wanafunzi hawa kukusanya taarifa rasmi za mitaro na baadhi ya wanajamii walitazama mchakato kama ni wa kisiasa, lakini wanafunzi walikua makini kuelezea lengo la mradi wa Ramani Huria kwa mtu yoyote alichunguza. 

Changamoto nyingine iliyojitokeza ni uelekeo wa maji katika mitaro. Wakati mwingine ni vigumu sana kuona upande upi maji yanaelekea. Tatizo hili lilitatuliwa kwa kuwauliza wanajamii kuhusu uelekeo wa mtaro husika au kwa kutizama kwa umakini katika mkusanyiko wa mchanga na uchafu.

Pia kulikuwa na changamoto ya usahihi wa mifumo ya GPS za simu za mkononi. Baadhi ya changamoto hizi zilitatuliwa na mtaalamu wa programu za kompyuta, Ka-Ping Yee kutoka nchini Marekani lakini kwa baadhi ya maeneo yalibaki kuwa tatizo, wakati wa upokeaji wa usahihi wa pointi ya GPS kwenye simu za mkononi.       

Mara kwa mara wanafunzi walikutana na upizani kutoka kwa wanajamii ambao hawakufahamu vizuri kuhusu mradi. Suala hili linaonyesha kwanini Ramani Huria ina msisitizo mkubwa katika uhusishwaji wa wanajamii.

Wanafunzi Wakiwa kata ya Hananasif

Licha ya matatizo machache, Wanafunzi walikusanya taarifa nyingi wawezavyo. Ripoti yao inaonyesha kuwa kuna mitaro mingi ambayo haijaungana, Mitaro yenye taka, na mitaa mingine haikuwa na mitaro kabisa-yawezekana kuwa ndio chanzo kikubwa cha mafuriko mabaya. 

Taarifa zilizokusanywa kwenye maeneo haya zinachambuliwa kwa usahihi kutumia programu ya QGIS. Wakati wa kuangalia data kupitia programu hii baadhi ya makosa yalijitokeza kama vile taarifa zilizokosekana na ambazo hazikuwa sahihi. Kwa kesi kama hizi, wanafunzi walienda kukusanya tena taarifa. Wakati mchakato unaendelea, wanafuzi wanaendelea kuelewa umuhimu wa kuangalia ubora wa taarifa wakati wa ukusanyaji

kisutu3.png

       Taarifa za mitaro ya Mtaa wa Kisutu Kata ya Hananasif  zikionyeshwa kwenye QGIS

Waanfunzi wetu wataendelea na mafunzo ya vitendo ili kuhakikisha wanakuwa na ujuzi unaohitajika wakati wa kufanya mchakato rasmi wa kutengeneza ramani.

Categories
Uncategorized

Kudhibiti Ubora Katika Kutengeneza Ramani za Mbali

Kupanua mradi wa kutengeneza ramani kwenye mji wenye watu zaidi ya milioni tano unahitaji mipango na mafunzo sahihi. Tulipenda kwanza wanafunzi wetu wapate  maelezo ya kina ya jinsi taarifa inaingizwa kwenye OSM ili kuhakikisha uelewa wazi wa mazingira ya OSM na jinsi inavyofanya kazi. Katika hatua ya baadaye, tutawaonyesha jinsi taarifa ya OSM inaweza kutumika kwa madhumuni kadhaa tofauti.

Kufundisha wanafunzi mia tatu kutengeneza ramani, huja na changamoto kadhaa. Wanafunzi  wetu wote ndio wanaanza, na wengi wao hawajawahi kuchangia kwenye OSM kabla. Kazi yao ya kwanza ilikuwa rahisi- kufungua akaunti za OSM, kusainiwa ili kujiunga na jamii ya kimataifa ya wachagiaji, tuliwaingiza kwenye jukwaa la OSM na kuwaonyesha jinsi ya kuhariri.

Moja ya malengo ya Ramani huria 2.0 ni kutengeneza ramani za jiji zima la Dar es Salaam kwenye OSM. Tulianza kwa kuwagawanya wanafunzi wetu kwenye makundi manne na kuwagawia kazi za ramani. Katika masaa machache, kazi ndogo sana zilifanywa  kwa asilimia mia moja, na wanafunzi walielekezwa kwa ufanisi jinsi ya kutengeneza ramani na walifanikiwa kuchangia kwenye OSM.

Tulitarajia wanafunzi wanaweza kusababisha makosa mbalimbali, na kweli ilikuwa hivyo – Ubora wa taarifa.

Jioni ile, tulipata ujumbe kutoka kwa moja kati ya wataalamu wenye uzoefu kwenye jamii ya OSM, ikionyesha baadhi ya makosa yaliyofanywa na wanafunzi wetu. Hii ndiyo nguvu ya jamii ya OSM. Mwanzoni wakati wa mafunzo, Swali liliulizwa kuhusu uhalisi wa taarifa za OSM na jinsi makosa yanavyotatuliwa na kudhibitiwa. Hili ndilo jibu, Jamii daima inaangalia taarifa hizi.

Wanafunzi wakichora ramani kutumia JOSM.

Kisha kwenye ajenda yetu ilikuwa kushughulikia maswala haya ya ubora wa taarifa, ambayo ni hatua muhimu katika kuchangia kwa ufanisi kwenye OSM. Masuala makuu yaliyotambuliwa yalikuwa makosa ya maandishi, majengo yasiyo na majina/sifa na majengo kadhaa ambayo hayajachorwa kwa ufasaha au majengo kushikamana. Tulitaka kuanzisha njia rahisi za kukabiliana na hili wakati pia tukitumia fursa ile ile kuonyesha thamani ya zana zaidi katika JOSM.

Josm filter ilisaidia kutatua changamoto za ubora wa taarifa, kwa mwongozo wa plugin kama orodha ya Todo. Mchanganyiko wa mambo haya ulituleta karibu kabisa katika kuondoa tatizo hilo. Timu zilihakiki kazi, ambazo zilipunguza na kuondoa baadhi ya makosa haya, lakini baadhi ya makosa hayakutatuliwa.

Kazi mpya ilianzishwa baadaye, iliyolenga  kuthibitisha taarifa ambayo iliundwa hapo awali.

Kazi mpya iliyotengenezwa.

Hatua za hili ni kama zifuatazo.

  • Chagua eneo la kuhakiki na fungua kwenye JOSM.
  • Tumia picha ya anga ya bing kuhakiki,kama inamawingu tumia Mapbox au DigitalGlobe Premium.
  • Angalia kama majengo yote yamechorwa kwenye sehemu unayofanyia kazi,kama kuna majengo ambayo hayajachorwa, yachore vizuri na yaandike building=yes.
  • Tumia filter kuficha barabara, matumizi ya ardhi, njia za maji. Ongeza filter zifuatazo kwenye JOSM.
  • type:node untagged (kuficha nukta zote ambazo hazina majina).
  • highway=* (kuficha barabara).
  • waterway=* (kuficha njia za maji).
  • landuse=* (kuficha matumizi ya ardhi).

Kutumia filters

  • Tumia Todo list plugin kuangalia sifa za jengo moja baada ya jingine.
    • Sifa za kuangalia ni;
      • building=yes                                          
  •  Makosa mengi yalikuwa yafuatayo;
    • buildin=yes
    • BUILDING=yes
    • Building=yes
    • building:=yes
    • builging=yes
    • bulding=yes
    • biuilding=yes
    • bubuilding:=yes
    • buildind=yes
    • builing=yes

Majengo yameongezwa kwenye orodha ya Todo ili kuchunguzwa 

  • Majengo yakisha hakikiwa (umbo na jina/sifa), thibitisha na angalia kama kuna kosa lolote na rekebisha.
  • Pakia kwenda kwenye OSM

Hatua hizi zilisuluhisha masuala kwa kiasi kikubwa. Hata hivyo, kulikuwa na baadhi ya makosa yaliyobaki hata baada ya kuangalia kazi tena. Tatizo sasa halikuwa lililohusiana na uendeshaji wa kazi, lakini kwa uzoefu. Wanafunzi wetu wanahitaji muda zaidi wa kufanya mazoezi ya kuchora  ramani ili kupunguza baadhi ya makosa haya ya ufanisi.

Tunazingatia pia kama swala la maandishi linaweza kuwa kipengele muhimu kwenye JOSM! Wachora  ramani mengi, hususan wapya, hufanya shughuli ndogo, kama vile kuongeza majengo; Wao mara chache huhutaji majina mengine ya kuweka nje ya majina ya msingi  ya kawaida ya OSM. Pengine JOSM ingeweza kuwakumbusha wachora ramani wakati lebo/jina lisio ndani ya JOSM (labda kutokana na makosa ya kimaandishi)? 

Kuna mtu/mtaalam yeyote kwenye jamii anataka kuangalia hili?

Categories
Uncategorized

Utengenezaji Ramani kwa Kasi

Timu mpya na iliyoongezwa ya Ramani Huria 2.0, yenye hadi zaidi ya wanafunzi mia tatu, kwa sasa ipo katika mazoezi ya vitendo ya kukusanya taarifa na kuhariri ramani ya kidigitali ya Dar es Salaam.

Tumeweka OpenDataKit (ODK), programu huru inayotumika kukusanya taarifa kwenye simu za smatifoni. Tutatumia mitandao mingine ya kisasa zaidi katika kukusanya taarifa kama vile OpenMapKit, programu ya haja ya ODK ambayo inaruhusu maingiliano ya moja kwa moja na taarifa za OpenStreetMap, lakini programu ya kuheshimika na yenye nguvu ya ODK ni nzuri kwa kuanzia. Tulianza kwa kufanya mazoezi ya vitendo kwenye viwanja kuzunguka dLab.

IMG_0431.JPG

Wanafunzi wakitumia ODK kwenye eneo la dLab.

Kwa kutumia ODK mtu yeyoye anaweza kuchukua pointi za GPS katika usahihi mzuri, na ya kutosha kwa aina nyingi za tafiti na pia kurekodi kwa kisasa majibu mengi kutoka kwenye utafiti ikiwemo maandishi, namba, machagulio kutoka kwenye orodha ya chaguzi, na hata pia picha! Uwezekano wa kukusanya taarifa iliyopangwa vizuri kwenye simu za mkononi ni ya kushangaza na kufurahisha, na wanafunzi wanashangaa wakati wa kuwaonyesha matokeo ya kazi yao kwenye ramani.

Water tank map at CoICT campus.jpeg

Taarifa za matenki ya maji zilizokusanywa na wanafunzi eneo la CoICT Chuo kikuu Cha Dar es salaam. 

Tuliwatuma wanafunzi nyumbani siku ya Ijumaa wakiwa na kazi ya mazoezi ya utafiti wa nyumbani, tukiwauliza kwenda kwa majirani zao mwishoni mwa wiki na kuuliza mfululizo wa maswali kuhusu aina gani ya nyumba watu wanaishi, kata na mitaa  wanayoishi, kama huwa wanapata mafuriko, jinsi/wapi wanapata maji, na aina ya vyoo wanavyotumia. Utafiti huu ni kwa ajili ya mazoezi ya vitendo (na wanafunzi wanaagizwa kuwaambia majirani zao hili ili kuhakikisha kwamba matarajio yasiyofaa hayaundwi), lakini inayotoa picha ya kushangaza na kufurahisha ya eneo kubwa  la Dar es Salaam. Kwa mshangao na furaha yetu, zaidi ya tafiti 900 zinakamilishwa mwishoni mwa wiki!

Household water sources zoomed image credit OSM.jpeg

Ramani ya Uchunguzi wa Kazi ya nyumbani, Inayoonyesha Chanzo cha Maji ya Kaya

Siku ya Jumatatu, tunatoka kwenye kumbi kubwa na kurudi kwenye madarasa manne Chuo Kikuu Ardhi, ambapo tulianza mafunzo kwa wanafunzi juu ya matumizi ya Java OpenStreetMap (JOSM), programu ambayo inaruhusu mtu yeyote aliye na kompyuta kuongeza taarifa kwenye OpenStreetMap. Ramani Huria ina nia ya kuweka kila jengo lililoko Dar es Salaam kwenye ramani, kwa hiyo tunaanza mara moja kwa kuchora majengo kutoka kwenye picha ya anga. Kuanzia Jumatatu mchana hadi jioni, wanafunzi 204 wenye kompyuta (kwa kusaidiwa na wanafunzi wengine mia moja ambao wanaangalia na kusaidia) waliongeza majengo zaidi ya 16,000 kwenye ramani! Wakati kuweka kila jengo katika mji kwenye ramani ni kazi kubwa, na hatujui kama tutaweza kufanya hivyo, lakini matokeo haya ya awali yanatia moyo sana.

IMG_0721.JPG
tasks coverage.jpeg

Picha ya ramani ya eneo lililochorwa.

Mwanafunzi akichora jengo

Mwishoni mwa siku ya Jumatatu, kwa kuhamasishwa na matokeo ya utafiti wa mazoezi ya wanafunzi, tunaanza jaribio muhimu; Je! Tunaweza kuimarisha wanafunzi wetu mia tatu waweze kutengeneza maelfu ya wana jamii watengeneza ramani? Tunawapatia vocha za simu za mkononi zenye muda wa maongezi, na kuwaelekeza wanafunzi kutafuta watu katika jumuiya zao, kuwapa vocha hizo, na kuwafundisha kupakua na kuweka ODK, na kujaza utafiti wa usajili. Jumanne asubuhi matokeo ya awali yameingia; wanajamii 170 walionyesha uwezo wa kujaza utafiti wa msingi na ODK kwa simu zao wenyewe! Wanafunzi, hata hivyo, hawakuridhika, wakasema kuwa wanaweza kufanya vizuri zaidi ikiwa wana muda zaidi. Leo tutamaliza swala la JOSM mapema na kuona jinsi watakavyofanya  hili.

Ndoto ya Ramani Huria, na kwa kweli ndoto ya miradi ya ramani ya wazi/huru kila mahali, ni kufanya ramani kuwa mchakato/mfumo shirikishi unaohusisha jumuiya nzima, ya kila mtu. Ikiwa wanafunzi wetu watakuwa na uwezo wa kufundisha na kuwawezesha wananchi kukusanya, kuelewa, na kutumia taarifa za mitaa katika jamii zao wenyewe, ni nani anayejua nini tunaweza kukamilisha?

Categories
Uncategorized

WANAFUNZI MIA TATU KUTENGENEZA RAMANI ZA KUZUIA MAFURIKO DAR ES SALAAM

Humanitarian Openstreet Team (HOT) na Ramani Huria, wakifadhiliwa na benki ya dunia na wadau wengine wameanzisha safari mpya na Chuo Kikuu Ardhi!

Wanafunzi mia tatu wa Mipango Miji na Geomatics kutoka Chuo Kikuu Ardhi jijini Dar es salaam wanashiriki katika mradi wa kutengeneza ramani za jamii mwezi Julai na Agosti.Tutatengeneza ramani za kata 35  jijini,msisitizo ukiwa katika taarifa zinazohitajika ili kuzuia mafuriko.

Kwa ongezeko la athari za mabadiliko ya tabia ya nchi na ukuaji wa miji, mafuriko mjini yamezidi kuvuruga na kutishia maisha ya watu wa Dar es Salaam. Ili kusaidia watu jijini, tutatengeneza ramani za mitaro, huduma za afya (muhimu kupunguza magonjwa na vifo endapo kutakuwa na mafuriko, hasa kwa watoto), vyoo, vyanzo vya maji, na miundombinu ya majengo.

Pia tutafanya kazi kuelewa wapi mafuriko yalitokea na wapi yanaweza kutokea mbeleni kwa kutegemea na ujuzi wa watu katika maeneo yao, pia na kupima mwinuko, na mfano wa mitaro itakavyokuwa na vingine.

Kufunza wanafunzi mia tatu katika kutengeneza ramani za kijamii ni changamoto kubwa na fursa! Kupanga kundi kubwa ni kazi/zoezi gumu. Lazima tuhakikishe wanafunzi wanapata ujuzi wenye tija, wanatengeneza taarifa zenye ubora wa hali ya juu, na kufanya kazi kwa ufasaha na wanajamii wanaowazunguka. Kwa bahati nzuri tuna timu inayojumuisha wanafunzi kumi wa zamani katika mradi uliopita wa Ramani Huria ambao wamehitimu na kuwa viongozi; watakuwa nguzo katika kuongoza wanafunzi wapya katika kujifunza njia za kutengeneza ramani.

Wanafunzi wakijifunza kuhusu Ramani Huria na wajibu wao katika mradi.

Kama kawaida, taarifa zinazokusanywa na Ramani Huria ni mali ya watu wa Dar es salaam. Ni taarifa huru, inayopatikana kwa yeyote katika jukwaaa la OpenStreetMap. Sio tu kuwa zinatumika katika mpango wa kupunguza mafuriko, uboreshaji huduma za afya, mitaro, na miundombinu mingine bali watu watazitumia katika njia za bure, ramani za bila mtandao kwenye simu zao za kidigitali na biashara ndogondogo zinaweza kutumia taarifa hizi kuboresha huduma kwa wateja. Ramani zenye ubora wa hali ya juu, zinazopatikana bure na kuwa na taarifa za mitaa zinasaidia karibia kila mmoja,na hasa pale zinapomilikiwa na watu wenyewe!

Kama upo Dar es salaam wiki chache zijazo, tegemea kuona timu yetu jiji zima la dar es salaam wakikusanya taarifa muhimu zitakazofanya jiji liwe bora, lenye nguvu, na sehemu makini. Na pia jaribu kutupia jicho kwenye ramani!